Tangaza Nasi

Mzee Mkapa na Mzee Kikwete waachwe wapumzike


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli amevionya vyombo vya habari vinavyowachafua Marais wastaafu, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete huku akivitaka viwaache wapumzike.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo ,Ikulu jijini Dar es salaam baada ya kukutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Barrick ya nchini Canada, Profesa John Thornton walipokutana kuzungumzia sakata la Makinikia.

“Nimesoma ripoti zote mbili hakuna mahali ambapo Mzee Mkapa na Mzee Kikwete wametajwa, vyombo vya habari viache kuwachafua hawa wazee, wamefanya kazi kubwa ya kulitumikia Taifa letu, viwaache wapumzike,” amesema Rais.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune


Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.