Tangaza Nasi

Niyonzima bado anamkataba na Yanga – Mkwasa



Mara baada ya dirisha la usajili kufumguliwa rasmi kumekuwa na mvutano mkubwa kwa baadhi ya majina makubwa ya wachezaji kuhusishwa kuhamia katika timu mbali mbali miongoni mwa majina ambayo yanaonekana kuteka vyombo vya habari katika kipindi hiki ni lile la kiungo wa klabu ya Yanga SC na Timu ya Taifa ya Rwanda, Haruna Niyonzima.

Kufuatia hilo Katibu Mkuu wa Klabu ya Yanga, Charles Boniface Mkwasa amewatoa hofu wanachama na mashabiki wa Yanga juu kiuongo wao Haruna Niyonzima ameyazungumza hayo kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram wa klabu hiyo

“Masuala ya Haruna nafikiri eeh pia niseme kama suala lake linafanana na masuala mengine yote ya usajili Haruna bado ni mchezaji wetu na mkataba wake bado haujamalizika”.

“Na natambua kwamba tayari tushampa taarifa ya kumalizana naye na kuzungumza naye katika masuala mazima ya usajili wake”.

 Kiungo wa klabu ya Yanga SC na Timu ya Taifa ya Rwanda, Haruna Niyonzima

“Nafikiri yeye aliaga hapa alienda kwenye National team, ninavyo fahamu mimi ameenda kwenye national team na ameahidi kurudi hapa tarehe 13 na atakapo rudi tutaendelea na mazungumzo naye”. Alisema Mkwasa ambaye ni Katibu Mkuu wa Klabu.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.