Tangaza Nasi

Real Madrid yampiga bei mtoto wa Zidane

REAL MADRID imeanza kuondosha watumishi hewa kwenye kikosi chake cha kwanza hii ni baada ya Jana usiku kumuuza kiungo wake,Enzo Zidane kwenda klabu ya Deportivo Alaves kwa ada ya uhamisho ambayo imefanywa siri.
Enzo ,22, ambaye ni mtoto wa kwanza wa kocha, Zinedine Zidane amejiunga na Deportivo Alaves kwa mkataba wa miaka mitatu wenye kipengele cha kurejea tena Real Madrid iwapo atahitajika hapo baadae.
Enzo anaihama Real Madrid akiwa amefanikiwa kuicheza mchezo mmoja  pekee msimu uliopita tena ikiwa dhidi ya Cultural Leonesa kwenye mchezo wa kombe la mfalme ambapo alifunga bao moja. 
Sehemu kubwa ya soka la Enzo limekuwa kwenye kikosi cha pili cha Real Madrid cha Castilla ambacho amekichezea michezo 78 na kufunga mabao saba. 
REAL MADRID imeanza kuondosha watumishi hewa kwenye kikosi chake cha kwanza hii ni baada ya Jana usiku kumuuza kiungo wake,Enzo Zidane kwenda klabu ya Deportivo Alaves kwa ada ya uhamisho ambayo imefanywa siri.
Enzo ,22, ambaye ni mtoto wa kwanza wa kocha, Zinedine Zidane amejiunga na Deportivo Alaves kwa mkataba wa miaka mitatu wenye kipengele cha kurejea tena Real Madrid iwapo atahitajika hapo baadae.
Enzo anaihama Real Madrid akiwa amefanikiwa kuicheza mchezo mmoja  pekee msimu uliopita tena ikiwa dhidi ya Cultural Leonesa kwenye mchezo wa kombe la mfalme ambapo alifunga bao moja. 
Sehemu kubwa ya soka la Enzo limekuwa kwenye kikosi cha pili cha Real Madrid cha Castilla ambacho amekichezea michezo 78 na kufunga mabao saba. 
 

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune

 

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.