Tangaza Nasi

Watu 19 wauawa mjini Mogadishu baada ya kushambuliwa na Al Shabab


Watu 19 wameuawa baada ya kundi la kigaidi la Al Shabab kutekeleza shambulizi la bomu mjini Mogadishu nchini Somalia.

Ripoti zinasema kuwa shambulizi hilo lilenga mkahawa maarufu katika mji huo mkuu.

Gari dogo lililokuwa limetegwa bomu lilipuka lakini pia magaidi hao kuwapiga risasi baadhi ya watu waliokuwa ndani ya mkahawa huo.

Abdi Bashir afisa wa usalama nchini humo amesema magaidi hao watano waliwazuia watu ndani na Mkahawa huo na kuanza kuwapiga risasi lakini wakalemewa.

Aidha amesema kuwa walifanikiwa kudhibiti mkahawa huo na kuwauwa magaidi watano.

“Tunadhibiti mkahawa na tumefanikiwa kumdhibiti mshambulizi huyu wa kujitoa mhanga,” ameimbia Reuters kupitia njia ya simu.

Kundi la Al Shabab, limedai kuhusika na shambulizi hilo.

Hii sio mara ya kwanza kwa mashambulizi kama haya kulenga mikahawa na maeneo mengine ya burudani nchini humo na kusababisha mauaji.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.