Korea Kaskazini yarusha kombora jingine la masafa marefu
Taarifa kutoka jeshi la Korea Kusini, zinabaini kwamba "kombora la masafa marefu lisilojulikana" lilirushwa kutoka eneo lililo karibu na mkoa wa Banghyon, magharibi mwa Korea Kaskazini.
Kombora hilo lilianguka katika Bahari ya Japan, kwa mujibu wa taarifa hizo.
Kombora hilo lililorushwa Jumanne
hii lilisafiri umbali wa kilomita 930 kwa dakika 40, kulingana na
taarifa kutoka Korea Kusini na Japan.
Korea Kaskazini imeongeza viwango vya majaribio vya makombora yake katika miezi ya hivi karibuni hatua inayoendelea kuzua hali ya sintofahamu.
Korea Kaskazini imeendelea na majaribio yake wakati ambapo Umoja wa Mataifa na Maekani wameendelea kuionya kutoendelea na mpango wake huo.
Mara ya mwisho Korea Kaskazini ilifanyia majaribio kombora lake mnamo mwezi Mei Ilirusha makombora yake katika wakati tofauti, yote yakielekezwa bahari ya Japan.
Wakati huo rais mpya wa Korea Kusini ameliomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuitisha mkutano wa dharura kuhusu swala hilo.
Korea Kaskazini imeongeza viwango vya majaribio vya makombora yake katika miezi ya hivi karibuni hatua inayoendelea kuzua hali ya sintofahamu.
Korea Kaskazini imeendelea na majaribio yake wakati ambapo Umoja wa Mataifa na Maekani wameendelea kuionya kutoendelea na mpango wake huo.
Mara ya mwisho Korea Kaskazini ilifanyia majaribio kombora lake mnamo mwezi Mei Ilirusha makombora yake katika wakati tofauti, yote yakielekezwa bahari ya Japan.
Wakati huo rais mpya wa Korea Kusini ameliomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuitisha mkutano wa dharura kuhusu swala hilo.


Post a Comment