Tangaza Nasi

Lacazette asaini mkataba wa miaka mitano Arsenal


Klabu ya Arsenal imekamilisha usajili wa mshambuliaji Alexandre Lacazette toka timu ya Lyon kwa dau la pauni Milioni 52.6 na kuvunja rekodi ya usajili ya timu hiyo.

Usajili wa kiungo wa Kijerumani Mesut Ozil ndio ulikua usajili wa bei ghali zaidi klabuni hapo aliposajiliwa mwaka 2013, kutokea Real Madrid kwa dau la pauni 42.4.

Lacazette amesaini mkataba wa miaka mitano kuwatumika washika mitutu hao wa London, mshambuliaji huyu atasafiri na timu wikiendi hii kuelekea Sydney kwa ajili ya michezo miwili ya kirafiki.

Msimu uliopita, Lacazette alikuwa mfungaji bora wa ligi ya Ufaransa alikozipasia nyavu mara 28 na ameshapiga jumla ya mabao 129 katika mechi 275 tangu alipoanza kuichezea timu ya kwanza msimu wa 2009/10.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.