Tangaza Nasi

Ray C kukesha studio siku mbili

Msanii wa Bongo Flava na hitmaker wa ngoma ‘Unanimaliza’, Ray C inaelezwa kutokana na uwezo wake wa kazi si ajabu yeye kukesha studio siku mbili akifanya kazi.

Mmoja wa mameneja wake, T Fighter ameeleza kwa malezi aliyolelewa Ray C ni tofauti na wasanii wengine kwani amezoea kurekodi albamu na si single.

“Tukienda studio tunakesha hata siku mbili, mimi nishazoea nikienda studio nakaa lisaa limoja naondoka ila yeye akiingia studio anakaa siku mbili anarekodi nyimbo tatu au nne kali,” ameiambia Planet Bongo ya EA Radio.

Ameongeza kuwa kutokana na uwezo wake wa kazi wimbo wa Unanimaliza ulirekodiwa ndani ya saa mbili tu.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune


Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.