Kesi ya Nondo kuletwa mashahidi watano April 18
Leo tarehe 10 April 2018 Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) na Mwanafunzi wa UDSM Abdul Nondo amefika mahakama ya Wilaya ya Iringa kwa ajili ya kusikiliza maelezo ya awali kuhusu kesi inayomkabili.
Akisoma mashtaka Upande wa Jamhuri Wakili wa Serikali Abel Mwandalamo amesema kuwa Nondo anakabiliwa na mashtaka mawili ambalo la kwanza ni kusambaza taarifa za uongo akiwa Ubungo jijiji Dar Es Salaam na kosa la pili ni kutoa taarifa za uongo akiwa mjini Mafinga kwa askari Polisi kituo cha Mafinga Wilayani Mufindi.
Nondo amekana mashtaka hayo yanayo mkabili mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya Wilaya ya Iringa Hakimu John Mpitanjia.
Aidha upande wa Jamhuri unakusudia kuleta mashahidi watano ambao ni Copro Salum, Veronica Fredy(Mpenzi wa Nondo), Alphonce Mwamule, Copro Abdulkadir na mtu kutoka Mtandao wa Tigo.
Kadhalika, upande wa jamhuri unakusudia kuambatanisha vielelezo vya ushahidi ambavyo ni Taarifa za uchunguzi kuhusiana na mawasiliano ya simu, Maelezo kutoka Mjini Mafinga yakidai Nondo katekwa na kuleta kielelezo cha simu za mkononi.
Upande wa Jamhuri umeomba kuanza usikilizwaji wa shauri hilo na watakuwa tayari kuleta mashahidi baada ya wiki moja.
Naye Hakimu John Mpita Njia amehairisha kesi hiyo na kuanza kusikilizwa tena mfululizo tarehe 18 na 19 kutokana na maombi ya upande wa utetezi wakili Chance Mloga kuiomba mahakama kusikiliza kesi hiyo kwa mfululizo.
Post a Comment