Tangaza Nasi

Brazil yaisamabaratisha Australia bao 4-0


                    " Brazil wakiwa ni wageni wamewatandika wenyeji Australia bao 4-0.."

Mechi za kirafiki za kimataifa kwa kalenda ya shirikisho la kandanda Ulimwenguni (Fifa) zimepigwa usiku wa kuamkia leo kwa Michezo kadhaa.

Nchini Australia ,Brazil wakiwa ni wageni wamewatandika wenyeji Australia bao 4-0 mbele ya Mashabiki wao lukuki.

Brazil wakicheza bila ya Nyota wao Neymar waliandika bao la kwanza kupitia Diego Souza na walifanikiwa kupachika Bao la Pili dakika ya 62 kupitia Thiago Silva na dakika ya 75 Taison akapachika bao la 3 na kisha Diego Souza kufunga ukurasa wa magoli kwa kuandika bao la nne dk 93 kipindi cha pili.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.