Khan asema hatomruhusu Trump kugawagawa Waingereza

Trump aaliandika kuwa Sadiq Khan alitoa sababu za uongo kwa kuwaambia wakazi wa London kwamba hakukuwa na sababu ya kuwa na wasiwasi.
Sadiq Khan amesema kuwa baadhi ya watu walionekana kuchochea mgawanyiko. Msemaji wa Ikulu ya Marekani, alikanusha rais kujipatia sifa kupitia jina la meya huyo ambaye ni muislam wa kwanza kushika wadhifa huo.
Sadiq Khan amsema akijitetea kwamba alisema kwamba watu hawakupaswa kuwa na wasiwasi baada ya kupelekwa askari wenye silaha mitaani katika jiji la London.
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa Mei amekosolewa kwa kupunguza 22% ya bajeti ya polisi wakati alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, kutokuwa makini kwa idara ya ujasusi pia kumewekwa mashakani. Umoja wa kitaifa uliyofuata mashambulizi ya Jumamosi usiku ulishindwa kwa shinikizo la uchaguzi ikiwa zimesalia siku tatu tu kabla ya uchaguzi wa wabunge wa mapema.
Shamblizi la mjini London Jumamosi Juni 3, lilisababisha vifo vya watu zaidi ya 48 na kuwajeruhi wengine wengi.
Post a Comment