Tangaza Nasi

Victor Wanyama autaja wimbo wa Bongo Flava anaoukubali


Mchezaji wa klabu ya soka ya Tottenham Hotspurs na timu ya taifa ya Kenya, Victor Wanyama, ameutaja wimbo wa Bongo Flava ambao anaupenda kwa sasa.

Akiongea katika kipindi cha Sports Extra cha Clouds FM, Wanyama ameutaja wimbo huo ni Orugambo wa Saida Karoli.

“Nafuatilia sana Bongo Flava na wasanii wote wanafanya vizuri kwasasa na nimependa wimbo huu mpya wa ‘Orugambo’ wa Saida Karoli,” amesema mchezaji huo.

Wanyama pia amefunguka kuwa alikuwa na nafasi kubwa ya kujiunga kuichezea Manchester United lakini dili hilo lilikuja kufeli baada ya Sir Alex Ferguson alipotangaza kustaafu kufundisha soka mwaka 2013.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.