Tangaza Nasi

Moto wateketeza soko kubwa zaidi nchini Zambia


Nchini Zambia soko kubwa zaidi nchini humo limeteketea moto.Soko hilo la City Market lililo mjini Lusaka, limekuwa likiteketea tangu mapema leo na limeteketeza badhaa nyingi zilizo kuwa katika soko hilo.

Walioshuhudia wanashuku kuwa moto huo ulisababishwa na hitilafu ya umeme na kuwalaumu wazima moto kwa kuchelewa kufika kuzuia moto huo kusambaa.

Mamlaka nchini humo bado zinachunguza chazo cha moto huo uliosababisha hasra kubwa kwa wafanya biashara wanaotumia soko hilo.

Soko hilo lina wafanyabiashara wengi zaidi nchini Zambia. Kati ya bidhaa zinazouuzwa ni pomoja na nguo za mitumba, vifaa vya elektroniki na hata chakula.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.