Tangaza Nasi

Wanajeshi 34 wa Cameroon hawajulikani waliko baada ya meli yao kuzama

Wanajeshi 34 wa Cameroon bado hawajapatikana, siku moja baada ya meli yao kuzama katika Pwani ya nchi hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita.

Ripoti zinasema kuwa, meli hiyo ilikuwa na abiria 37 ikielekea katika mji wa Bakassi.

Waziri wa Ulinzi Joseph Beti Assomo amesema wanajeshi watatu ndio waliokolewa wakiwa hai baada ya kuzama kwa meli hiyo.

“Wanajeshi 34 bado hawajukani waliko lakini watatu wameokolewa,” amesema Waziri Assomo.
Meli hiyo ilikuwa imewabeba wanajeshi wa nchi hiyo wanaoaminiwa kupambana na kundi la Boko Haram kutoka nchini Nigeria Kaskazini mwa nchi hiyo.

Wizara ya ulinzi nchini Cameroon imesema meli hiyo ilipoteza mawasiliano kuanzia mapema wakati ikitokea jijini Duala ikielekea Bakasi saa moja kabla ya kupoteza mawasiliano.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.