Tangaza Nasi

Majibu ya Jux alipoulizwa kama anaweza kujiunga WCB

Msanii wa Bongo Flava, Jux amesema anaweza kujiunga na record label yoyote endapo watafikia makubaliano ila sio kitu ambacho amekifikiria kwa sasa.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Utaniua’ ameiambia Planet Bongo ya EA Radio Wasafi record ni label nzuri ila hajawahi kuongea kitu kama hicho.

“Ni kitu kizuri sio kibaya kwa sababu ile ni record label, hiyo nafasi ikipatika sio mbaya lakini kwa mimi sikuwahi kufikiria kwa hapa Tanzania au kwa Africa kwa kweli,” amesema.

“Iwe ni kampuni au sehemu ambayo itanichukua mimi kama kunimeneji pale nilipokuwa wafanye vitu extra zaidi. Sawa wanaweza ikawa wanaweza kwa mkataba kama watakuja na mkataba ambao nitautaka na vitu vyangu ambavyo navihitaji naweza nikasaini kwa sababu mimi ni mfanyabiashara lakini kwa sasa hivi hatukuwahi kuongea au kufikiria,” ameongeza.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune




Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.