Tangaza Nasi

AU: Uhuru na Raila hawakubaliani juu ya utayarishaji wa uchaguzi


Umoja wa Afrika unasema rais Uhuru Kenyatta na Mgombea mkuu wa upinzani Raila Odinga wanatofautiana kuhusu maandalizi na utayari wa Tume ya Uchaguzi kusimamia Uchaguzi Mkuu mwezi ujao.

Hili limebainika baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Umoja huo Moussa Faki Mahamat kumaliza ziara yake nchini humo baada ya kukutana na viongozi hao wawili, mashirika ya kiraia na Tume ya Uchaguzi.

Odinga amekuwa akihoji utayari wa tume ya Uchaguzi, huku rais Kenyatta akisisitiz akwua ni lazima Uchaguzi ufanyike tarehe nane mwezi ujao na kuwashtumu wapinzani kutaka uchaguzi huo kuahirishwa.

Kiongozi wa waangalizi wa Umoja wa Afrika ambaye ni rais wa zamani wa Afrika Kusini Thambo Mbeki amesema wamekutana na wadau mbalimbali kuhakikisha kuwa maandalizi yanakuwa mazuri.

Siku ya Alhamisi Mahakama ya rufaa iliamua kuwa tume ya Uchaguzi inaweza kuendelea kuchapisha karatasi za kuwania urais . Haijabainika ikiwa upinznai utakataa rufaa katika Mahakama ya juu.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune


Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.