Tangaza Nasi

Vijana 6 kutoka Burundi watoweka Marekani


Taarifa kutoka vyombo vya usalama nchini Marekani zinabaini kwamba vijana sita kutoka Burundi waliokuwa wakishiriki katika mashindano ya roboti nchini Marekani wametoweka, na haijulikani walipo, taarifa ambayo haijathibitishwa na serikali ya Burundi.

Waandalizi wa mashindano hayo wanasema kuwa waliwaeleza polisi baada ya msimamizi wa timu hiyo ya Burundi kushindwa kuwapata vijana hao.

Idara ya polisi mjini humo imesema kuwa mara ya mwisho vijana hao kuonekana ilikuwa siku ya Jumanne wakati wa makamilisho ya michezo hiyo.

Vijana hao ambao ni wavulana wanne na wasichana 2 walio kati ya umri wa miaka 16 na 18 walipotea wakati wa mashindano hayo ya kwanza duniani yaliofanyika Washington DC.

Vijana hao wanatambulika kuwa Don Ingabire, Kevin Sambukiza, Nice Munezero, Audry Mwamikazi, Richard Irakoze na Aristide Irambona.

Kulingana na gazeti la The Washington Post, msemaji wa mashindano hayo Jose Escotto alisema, ripoti kamili imewasilishwa kwa polisi ambao wanachunguza kisa hicho.

Mashindano hayo yyaliyohudhuriwa na timu 150 yanalenga kuwashawishi vijana kukuza vipaji vyao katika masomo ya sayansi, technolojia, uhandisi na hesabu.

Taarifa zaidi kutoka yombo vya usalama zinasema kuwa vijana wawili kati yao tayari wamevuka mpaka na kuingia nchini Canada.

Idara ya polisi ilibandika picha za sura za vijana hao sita waliopotea katika mtandao wao wa Twitter.

Polisi imewataka raia kuwasiliana nao iwapo watakuwa na habari yoyote kuhusu vijana hao.

Jiunge na BongoTune sasa 

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,  na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Bongo Tune


Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.