Tangaza Nasi

Muigizaji maarufu nchini India Salman Khan afungwa jela


Mahakama nchini India imemhukumu muigizaji maarufu nchini humo, Salman Khan, kifungo cha miaka mitano jela baada ya kumkuta na hatia ya kufanya ujangili na kumuua swala paa kinyume cha sheria.
Mahakama ya Jodhpur imetoa hukumu hiyo leo kufuatia kosa hilo ambalo Khan anadaiwa kulifanya mwaka 1998 alipokuwa anatayarisha filamu yake Magharibi mwa jimbo la Rajasthan.
Mbali na hukumu hiyo ya kifungo jela, mahakama pia imempiga faini ya repee 10,000 (sawa na $154). Khan amechukuliwa kupelekwa gerezani muda mfupi uliopita.
Hii ni kesi ya nne aliyowahi kufunguliwa muigizaji huyo kwa madai ya kufanya ujangili dhidi ya wanyama pori alipokuwa anatayarisha filamu yake ya Hum Saath Saath Hain, mwaka 1998.

Hakuna maoni

Inaendeshwa na Blogger.