Man City wakamilisha kumnunua Kyle Walker kutoka Tottenham
Manchester City wamekamilisha ununuzi wa beki wa kulia wa Tottenham na England Kyle Walker kwa kitita cha £45m.
Uhamisho wake, ambao unakuwa na jumla ya £50m ukiongeza kikolezo cha £5m, huenda ukamfanya kuwa mchezaji ghali zaidi wa England kuwahi kuwepo.
"Nina furaha sana kujiunga na City na nasubiri sana kuanza kucheza," amesema Walker.
"Pep Guardiola ni miongoni mwa mameneja wanaoheshimiwa zaidi duniani."
Walker alijiunga na Spurs kutoka Sheffield United mwaka 2009 na amecheza mechi 183 Ligi ya Premia.
Katika Manchester City atavalia jezi nambari mbili.
Anatarajiwa kusafiri na City Jumatatu kwa ziara yao ya Marekani.
Wachezaji ghali zaidi wa Uingereza
| £85.3m - Gareth Bale (Tottenham kwenda Real Madrid, 2013) | |
| £49m - Raheem Sterling (Liverpool kwenda Manchester City, 2015) | |
| £47.5m - John Stones (Everton kwenda Manchester City 2016) | |
| £45m - Kyle Walker (Tottenham kwenda Manchester City 2017) | |
| £35m - Andy Carroll (Newcastle kwenda Liverpool, 2011) |


Post a Comment